Thursday, July 24, 2014

NI KATIKA JUKWAA LA SANAA BASATA






JE WA SANII WANAJUA UMUHIMU WA BIMAA?


MANUFAA YA BIMA KWA WASANII

Na AGNES MHAGAMA

  Kwakupitia  programu  ya  kila wiki  Baraza la sanaa (BASATA)  limetoa  elimu  kwa wadau wa sanaa  na wasanii  kuhusu  umuhimu wa kuwa na bima kwa  ajiri  ya ulinzi wa afya zao pamoja na mali zao.

Hayo  yamebainishwa na Afisa  masoko   wa kampuni ya MGEN  inayojishughulisha na mambo ya bima na Bw.JAFARRY JUMBE wakati akiongea na wasanii pamoja na wadau wa sanaa katika  Jukwaa la  sanaa  jijini Dar es salaam.

Bw.jumbe alisema  wasanii watafaidika  na huduma hiyo popote watakapo kama vile,msanii akipata matatizo ya ajali, kuungua kwa mali zake, kupatwa na maradhi    , kama kampuni ya MGEN  itahusika na ulipaji wote wa awali  wa mali yake.

Aliongeza kwamba, msanii kuwa na bima ni mhimu kwani katika kazi zake za kukuza sanaa anakumbana na changamoto mbalimbali kwahiyo  kama atakuwa na Bima ita msaidia yeye kuweza kufidia baadhi ya sehemu atakazo kuwa ameshindwa kutekeleza.
Hatahivyo alisema kampuni imeamua  kugawa bima kwa ngazi mbalimbali  ilikulahisisha kila mtu aweze kuwa na bima mojawapo  kama  bima ya mtu mmoja, bima ya vikunndi vya watu ,bima ya mali ,ili  kumsaidia msanii aweze kuwa na bima itakayo msaidia katika ulinzi wa mali zake kwa haraka zaidi.

Licha ya hayo aliwataka wasanii kutokuwa na hofu ya gharama  na kuepuka maneno ya mitaani yanayo  toa taarifa za uongo juu ya  huduma hiyo kwani kampuni hiyo imeweza kuweka gharama ndogo zitakazo mfanya mtu yoyote aweze kukidhi.




                            

Tuesday, July 15, 2014

PICHA ZA JUKWAA NA TOUR YA MWANDISHI WETU CHECK!!!



































UNA WEZA JARIBUUUU!!!



NI MWENDO WA SARAKASIIIII!!








USHAWAHI ONAAA!!!


habarika na agnes mhagama



WASANII WA SARAKASI WA ILALAMIKIA SERIKARI

Kampuni ya Simple Entertainment inayo jishughulisha na kuinua vipaji vya sarakasi  ndani ya nchi na nje ya nchi  imeiomba serikari kutupia jicho sanaa hiyo  kwani imekuwa ikisahaulika na kutothamini wa katika sanaa hiyo,licha ya kuwa imekuwa ikifanya kazi kubwa ya  mchango wa kuitambulisha nchi   na kutangaza  katika mataifa mbalimbali duniani.

Hayo yamezungumzwa hivi karibuni  na mkurugenzi wa kampuni hiyo Bwana Jacob Chinunda, wakati akizungumza na wasanii pamoja na wadau wa sanaa  katika kongamano la kila wiki la jukwaa la sanaa  linaloendeshwa na Baraza la sanaa la taifa (BASATA) jijini Dar es salaam.

Chinunda alisema sanaa ya sarakasi ina bidi ithaminiwe na kuwekewa mkazo kama sanaa nyingine , kwani ni sanaa ya kipekee ambayo imekuwa ikitambulisha nchi katika mataifa mbalimbali kupitia maonyesho ambayo wanakuwa wakifanya, kutokana na soko dogo la nchi yetu na kutothaminiwa sanaa hiyoimekuwa ikifanya na kuchezwa kila mara nje ya nchi kwa lengo la kutafuta masoko na kupendwa zaidi na watu wa nje ya nchi.

“wasanii wa sarakasi wamekuwa wakipata shida nyigi katika kupata ma agence kwani kwa nchi yetu  ni wachache sanaa ,mpaka uwe agence nilazima uwe msanii wa sarakasi,kadri siku zinavyo zidi kwenda wasanii hao wamezidi kupotea na kukatatamaa ya sanaa hiyo kulingana na changamoto wanazo kumbana nazo”alisema.

Aliongeza kwamba, sanaa hiyo imekuwa ikitambulisha vizuri jina la Tanzania  kwani kila wanapotaka kufanya  onyesho ni lazima  upeperushe bendela ya nchi yako ikiwa ni utambulisho wa sehemu uliyo toka,hali hiyo imepelekea kwa watalii wengi kupenda kuja Tanzania kwa ajili ya kujionea maonyesho hayo ya aina yake.

Licha ya hayo  alieleza changamoto wanazo kumbana nazo ikiwemo na serikali kuwasahau kwani imepelekea sanaa hiyo kuto endelea na kufahamika zaidi kimataifa na dunia nzima kama ikiwemo usumbufu mkubwa wanapokuwa wanasafiri,wanapokuwa wanataka bendera ya taifa imekuwa nitatizo kwani hadi  ina wa gharimu kutafuta vitambaa na kutengeneza bendea li iweishara ya utambulisho wan chi wanayotokea.

Monday, July 14, 2014

WAFAHAU WENGI KUPITIA HAPA


LEO KATIKA JUKWAA LA SANAA




UTAWEZA KUFAHAMU MAMBO MENGI  YANAYO HUSU CHANGAMOTO, FURSA NA MAENDELEO YA SANAA ZA SARAKASI HAPA NCHINI

USIKOSEE KUFIKA KATIKA JUKWAA LA SANAA  BASATA

Sunday, July 13, 2014

SANAA YETU INAENDA WAPI



SANAA YETU INASONGA MBELE AU INAANGAMIA
Sito acha kusahau maneno ya wahenga wetu  kwani walisema  (YA KALE NIDHAHABU) wakiwa na maana  ya kituchochote cha nyuma ni bora zaidi kuliko kipya, kwani kuna watu wakiona wamepata kitu kipya basi wana dharau kitu cha nyuma.,Au kulingana na utandawazi utaona mambo yakale yakiwa mstari wa nyuma sana na kusahaurika na  kuona hayana maana  na kuendeleza  mambo ya kisasa na kusahau kabisa ubora wa mambo ya nyuma.
Msomaji wangu nazungumzia tasnia ya sanaa toka enzi za miaka ya 79 kurudi nyuma  kiukweli tamaduni za asili zilikuwa zina pamba moto na enzi hizo tulikuwa tunajivunia sanaa yetu ,sio sasa yani kadri siku zinavyoenda na pata machungu sana ninavyoona asili yetu inapotea siku hadi siku na kusahau  kabisa kama inabidi tuukuze utamaduni wetu na sio kuacha watu wakautumie utamaduni wetu.
Miaka ya nyuma tukiangalia bendi za muziki kama  sikinde,msondo,resiwanyika kweli tunaona mashairi yaliyo pangwa kwa vina na ukisikiliza unapata mafunzo mengi bila kujari unasikiliza na nani. Kiukweli miaka ya nyuma tukizungu mzia mziki tunayo ya kuzungumza lakini kwa sasa nashidwa nianzie wapi kwani kumekuwa na miziki ya aina nyingi na kila mziki una staili yake na suala la kitamatuni au maadili halija wekewa mkazo sana na kudharaulika kabisa.
Nikiangalia hali ya sanaa ya sasa naona itakuja kufika sehemu suala la utamaduni likapotea kabisa kwani kwa sasa kila mtu anajaribu kufanya mziki kulingana nay eye anataka nini na si kuangalia je niwatu gani watakwenda kusikiliza au kuangalia kazi yangu , jambo hilo linasikitisha sana kwani kuna baadhi ya nyimbo na video za muziki zinapotosha kabisa ukiangalia kama mtu mzima umekaa na watoto itabidi usimame na kutoka nje je/ halihiyo inapeleka wapi tamaduni  yetu. Ni tuna kuza au kubomoa?
Kama wasanii ina bidi tufike mahari na kubadilika na kujalibu kuangalia wapi tuliko toka na wapi tunaenda ili kuhakikisha kazi zetu zinafika sehemu nzuli na kuweza kufahamika mataifa na mataifa ,lakini kama utaendeleza kuharibu kwa kufanya sanaa za ajabu kama ngoma za vigodoro, ngoma za kanga moja  na nyingine zinazo vunja utamaduni hatuta songa mbele na tutaibua tamaduni nyingine ni mhimu kutunza tamaduni zetu. Msomaji kwaleo ni hayo tuu panapo majariwa tutaendelea