Thursday, July 24, 2014
JE WA SANII WANAJUA UMUHIMU WA BIMAA?
MANUFAA YA BIMA KWA
WASANII
Na AGNES MHAGAMA
Kwakupitia
programu ya kila wiki Baraza la sanaa (BASATA) limetoa elimu
kwa wadau wa sanaa na wasanii kuhusu umuhimu wa kuwa na bima kwa ajiri
ya ulinzi wa afya zao pamoja na mali zao.
Hayo yamebainishwa na
Afisa masoko wa
kampuni ya MGEN inayojishughulisha na
mambo ya bima na Bw.JAFARRY JUMBE wakati akiongea na wasanii pamoja na wadau wa
sanaa katika Jukwaa la sanaa jijini Dar es salaam.
Bw.jumbe alisema wasanii watafaidika na huduma hiyo popote watakapo kama
vile,msanii akipata matatizo ya ajali, kuungua kwa mali zake, kupatwa na
maradhi , kama kampuni ya MGEN itahusika na ulipaji wote wa awali wa mali yake.
Aliongeza kwamba, msanii kuwa na bima ni mhimu kwani katika
kazi zake za kukuza sanaa anakumbana na changamoto mbalimbali kwahiyo kama atakuwa na Bima ita msaidia yeye kuweza
kufidia baadhi ya sehemu atakazo kuwa ameshindwa kutekeleza.
Hatahivyo alisema kampuni imeamua kugawa bima kwa ngazi mbalimbali ilikulahisisha kila mtu aweze kuwa na bima
mojawapo kama bima ya mtu mmoja, bima ya vikunndi vya watu
,bima ya mali ,ili kumsaidia msanii
aweze kuwa na bima itakayo msaidia katika ulinzi wa mali zake kwa haraka zaidi.
Licha ya hayo aliwataka wasanii kutokuwa na hofu ya gharama na kuepuka maneno ya mitaani yanayo toa taarifa za uongo juu ya huduma hiyo kwani kampuni hiyo imeweza kuweka
gharama ndogo zitakazo mfanya mtu yoyote aweze kukidhi.
Tuesday, July 15, 2014
habarika na agnes mhagama
WASANII WA SARAKASI WA ILALAMIKIA SERIKARI
Kampuni ya Simple Entertainment inayo jishughulisha na kuinua vipaji
vya sarakasi ndani ya nchi na nje ya
nchi imeiomba serikari kutupia jicho
sanaa hiyo kwani imekuwa ikisahaulika na
kutothamini wa katika sanaa hiyo,licha ya kuwa imekuwa ikifanya kazi kubwa ya mchango wa kuitambulisha nchi na kutangaza katika mataifa mbalimbali duniani.
Hayo yamezungumzwa hivi karibuni
na mkurugenzi wa kampuni hiyo Bwana Jacob Chinunda, wakati akizungumza
na wasanii pamoja na wadau wa sanaa
katika kongamano la kila wiki la jukwaa la sanaa linaloendeshwa na Baraza la sanaa la taifa (BASATA)
jijini Dar es salaam.
Chinunda alisema sanaa ya sarakasi ina bidi ithaminiwe na kuwekewa
mkazo kama sanaa nyingine , kwani ni sanaa ya kipekee ambayo imekuwa
ikitambulisha nchi katika mataifa mbalimbali kupitia maonyesho ambayo wanakuwa
wakifanya, kutokana na soko dogo la nchi yetu na kutothaminiwa sanaa
hiyoimekuwa ikifanya na kuchezwa kila mara nje ya nchi kwa lengo la kutafuta
masoko na kupendwa zaidi na watu wa nje ya nchi.
“wasanii wa sarakasi wamekuwa wakipata shida nyigi katika kupata ma
agence kwani kwa nchi yetu ni wachache
sanaa ,mpaka uwe agence nilazima uwe msanii wa sarakasi,kadri siku zinavyo zidi
kwenda wasanii hao wamezidi kupotea na kukatatamaa ya sanaa hiyo kulingana na
changamoto wanazo kumbana nazo”alisema.
Aliongeza kwamba, sanaa hiyo imekuwa ikitambulisha vizuri jina la Tanzania
kwani kila wanapotaka kufanya onyesho ni lazima upeperushe bendela ya nchi yako ikiwa ni
utambulisho wa sehemu uliyo toka,hali hiyo imepelekea kwa watalii wengi kupenda
kuja Tanzania kwa ajili ya kujionea maonyesho hayo ya aina yake.
Licha ya hayo alieleza
changamoto wanazo kumbana nazo ikiwemo na serikali kuwasahau kwani imepelekea
sanaa hiyo kuto endelea na kufahamika zaidi kimataifa na dunia nzima kama
ikiwemo usumbufu mkubwa wanapokuwa wanasafiri,wanapokuwa wanataka bendera ya
taifa imekuwa nitatizo kwani hadi ina wa
gharimu kutafuta vitambaa na kutengeneza bendea li iweishara ya utambulisho wan
chi wanayotokea.
Monday, July 14, 2014
WAFAHAU WENGI KUPITIA HAPA
LEO KATIKA JUKWAA LA SANAA
UTAWEZA KUFAHAMU MAMBO MENGI YANAYO HUSU CHANGAMOTO, FURSA NA MAENDELEO YA SANAA ZA SARAKASI HAPA NCHINI
USIKOSEE KUFIKA KATIKA JUKWAA LA SANAA BASATA
Sunday, July 13, 2014
SANAA YETU INAENDA WAPI
SANAA YETU INASONGA MBELE AU INAANGAMIA
Sito acha kusahau maneno ya wahenga
wetu kwani walisema (YA KALE NIDHAHABU) wakiwa na maana ya kituchochote cha nyuma ni bora zaidi
kuliko kipya, kwani kuna watu wakiona wamepata kitu kipya basi wana dharau kitu
cha nyuma.,Au kulingana na utandawazi utaona mambo yakale yakiwa mstari wa
nyuma sana na kusahaurika na kuona
hayana maana na kuendeleza mambo ya kisasa na kusahau kabisa ubora wa
mambo ya nyuma.
Msomaji wangu nazungumzia tasnia ya
sanaa toka enzi za miaka ya 79 kurudi nyuma kiukweli tamaduni za asili zilikuwa zina pamba
moto na enzi hizo tulikuwa tunajivunia sanaa yetu ,sio sasa yani kadri siku
zinavyoenda na pata machungu sana ninavyoona asili yetu inapotea siku hadi siku
na kusahau kabisa kama inabidi tuukuze
utamaduni wetu na sio kuacha watu wakautumie utamaduni wetu.
Miaka ya nyuma tukiangalia bendi za
muziki kama sikinde,msondo,resiwanyika
kweli tunaona mashairi yaliyo pangwa kwa vina na ukisikiliza unapata mafunzo
mengi bila kujari unasikiliza na nani. Kiukweli miaka ya nyuma tukizungu mzia
mziki tunayo ya kuzungumza lakini kwa sasa nashidwa nianzie wapi kwani kumekuwa
na miziki ya aina nyingi na kila mziki una staili yake na suala la kitamatuni au
maadili halija wekewa mkazo sana na kudharaulika kabisa.
Nikiangalia hali ya sanaa ya sasa
naona itakuja kufika sehemu suala la utamaduni likapotea kabisa kwani kwa sasa
kila mtu anajaribu kufanya mziki kulingana nay eye anataka nini na si kuangalia
je niwatu gani watakwenda kusikiliza au kuangalia kazi yangu , jambo hilo
linasikitisha sana kwani kuna baadhi ya nyimbo na video za muziki zinapotosha
kabisa ukiangalia kama mtu mzima umekaa na watoto itabidi usimame na kutoka nje
je/ halihiyo inapeleka wapi tamaduni
yetu. Ni tuna kuza au kubomoa?
Kama wasanii ina bidi tufike mahari
na kubadilika na kujalibu kuangalia wapi tuliko toka na wapi tunaenda ili
kuhakikisha kazi zetu zinafika sehemu nzuli na kuweza kufahamika mataifa na
mataifa ,lakini kama utaendeleza kuharibu kwa kufanya sanaa za ajabu kama ngoma
za vigodoro, ngoma za kanga moja na
nyingine zinazo vunja utamaduni hatuta songa mbele na tutaibua tamaduni
nyingine ni mhimu kutunza tamaduni zetu. Msomaji kwaleo ni hayo tuu panapo
majariwa tutaendelea
Subscribe to:
Posts (Atom)