makala


WASANII WANAJUA UMUHIMU WA JUKWAA LA SANAA?
Nimekuwa nikihudhuria konga mano la Jukwaa la sanaa kila wiki kama ilivyo pangwa na Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA),kwalengo la kujifunza mambo mbalimbali yanayo husu sanaa na wasanii ,pia kwa kupitia Jukwaa hilo nime weza kuwafahamu wadau mbalimbali na wasanii mbalimbali.
Katika Jukwaa la sanaa kawaida yake huwa kuna kuwa na mada zilizo andaliwa na wataalamu mbalimbali ambao wanakuwa wamechanganua nakufika maamuzi ya kuliweka mezani ili wasanii waweze kujifunza pamoja na wadau wa sanaa waweze kuchangia  madahiyo ambayo inakuwa mezani.
Kama Basata imetambua umuhimu wa kuanzisha Jukwaa hilo ,na ninaamini kilakitu kinachokuwa kimewekwa basi kina wekwa kwa malengo maalumu na kina kuwa nasababu maalumu zinazopelekea kuwepo kwakitu cha namuna hiyo,kwa upande wangu nina ipongeza Basata kwa kuanzaa programu hiyo kwani maono yangu kwa kupitia Jukwaa hilo wasanii watapata fursa za kujifunza mambo mbalimbali.
Nakumbuka kuna mada moja ambayo nilivutiwa nayo sana mada iliyokuwa ikizumzia juu ya ‘’kwa nini watanzania wengi wanathamini kazi za wasanii wa nje na kudharau au kuto kuthamini kazi zetu sisi wenyewe tunazo zitengeneza wenyewe kama Muziki na filamu’’
Mada hiyo ilinivutia sana na waendesha mada waliweza kuichambua vizuri sana,lakini kilicho ni sikitisha nikwamba walengwa wenyewe hawakuwepo ,jambo lililo nipa maswali mengi na kupata uchungu kwamba Basata imeandaa mada kwa kuamini au kwa dhumuni kubwa la walengwa waweze kufikiwa na mada hizo ili kama kunakuwa na vitu vya wasanii kubadirika basi waweze kufanya kitu chatofauti, nasio kuona mabadiliko katika sanaa yana baki yaleyale na kusababisha sanaa kuto kukua bali kupotea kabisa.
Idadi ya wasanii kuhudhuria katika Jukwaa la sanaa imekuwa ndogo sana wakati mwingine hakuna msanii yeyote ambaye ni maalufu anayeweza kuja jambo ambalo linalo pelekea dhumuni la kuweka Jukwaa hilo kuto tiliwa maanani, kwani wasanii chipukizi ndio ambao wanahudhulia , jambo ambalo wasanii hao chipukizi wanajifunza kutoka kwa wasanii wanao fahamika namaanisha maarufu.
Kunapotokea matatizo ya sanaa au kazi ya sanaa kuto kwenda vizuri ambao wanakuwa wamefanya ni hao wasanii.chaajabu Basata inapoona hayo na kuamua Kuandaa mada ya kuweza kutatua hilo tatizo au kusikiliza wasanii kama wa sanii wanataka nini ,utaona hawahudhurii katika Jukwaa la sanaa na kupuuza.
Kinacho nishangaza nikwamba kwenye vitu mhimu kama hivi vya kujadili mada ukiwahusisha wa sanii hawafiki katika Jukwaa sijajua nini tatizo la wasanii ni kudharau mada?au nini lakini katika Maonyesho mengine ambayo sio mhimu uta wakuta wakiwekea kipaumbele.
Wito wangu wasanii ebu tambueni umuhimu wa kuwa najukwaa hilo kwani ni muhimu na lina faida .kuliko kuendelea kulalamika na kulaumu pasipo kuja wenyewe kwenye Jukwaa muweze kuchangia hoja na kujifunza mambo mengine mazuri ya kufanya tasnia yetu ya sanaa isonge mbele.




No comments:

Post a Comment