Wednesday, April 30, 2014

FAINALI LA KOMBE LA UEFA MJINI LONDONI NINI KIMEJILI


Fainali na Real ni Chelsea au Atletico?

 
John Terry nahodha wa Chelsea
Nahodha wa Chelsea John Terry na Eden Hazard watakuwa tayari katika kikosi cha Jose Mourinho kitakachocheza dhidi ya Atletico Madrid katika mchezo wa marudiano hatua ya nusu fainali ya Kombe la UEFA mjini London, Jumatano.
Hata hivyo mlinda mlango tegemeo wa Chelsea, Petr Cech hatajumuishwa kwenye kikosi hicho kutokana na kuwa majeruhi.
Terry aliumia kifundo cha mguu katika mchezo wa kwanza uliomalizika kwa kutofunganauku Cech akiteguka bega.Mark Schwarzer ambaye amekuwa akifanya vizuri langoni tangu kuumia kwa Cech ataendelea kulilinda lango la Chelsea.
Wachezaji wa Atletico Madrid wakifurahia goli
Hazard, atacheza kwa mara ya kwanza tangu Aprili 8 na Samuel Eto'o naye ni imara kuweza kucheza mchezo huo.
Nahodha wa Atletico Gabi anatumikia adhabu ya kadi, ambapo mchezaji kiungo wa zamani wa Chelsea Tiago Mendes anatarajiwa kuchukua nafasi yake.
Swali linalobaki ni nani kati ya Chelsea na Atletico atakayeungana na Real Madrid kucheza fainali ya UEFA mwaka 2014 mjini Lisbon? Real imefuzu kucheza fainali za UEFA mwaka huu baada ya kuisambaratisha Bayern Munich kwa jumla ya mabao 5-0 na hivyo kuivua rasmi ubingwa na kuliacha kombe hilo likiwaniwa na timu mpya.

JE WAJUA????




Nigeria:Maandamano dhidi ya serikali

Maandamano kuhusu wasichana waliotekwa
Maandamano makubwa ya kwanza yanatarajiwa kufanyika katika mji mkuu wa Nigeria- Abuja baadaye leo watu wakiitaka serikali kuchukua hatua zaidi kuwanusuru wasichana 200 wa shule waliotekwa nyara na wanamgambo wa kiislam .
Wasichana hao walichukuliwa kutoka shule yao ya malazi iliyopo katika eneo lisiloweza kufikiwa kwa urahisi kaskazini mashariki mwa nchi zaidi ya wiki mbili zilizopita.
Waandalizi wa maandamano hayo wanaita serikali kuelekeza juhudi zao kwa wasichana waliopotea .
Mpango ni kuandamana hadi bungeni na kwa mshauri wa taifa wa masuala ya usalama na kuwasilisha barua ya kutoa wito wa kufanyika kwa juhudi zaidi kuwanusuru wasichana hao.
Mwanaharakati mmoja wa kijamii amesema katika nchi nyingine yoyote ile suala la kutekaji nyara wa wasichana hao wengi lingekuwa ni mjadala wa kila siku .
Lakini serikali ya Nigeria imekuwa ikikabiliwa na ukosoaji mkubwa kwa kukaa kimwa huku wazazi wenye shauku wakisailia kuwa gizani kuhusu nini kinachoendelea kuhusiana na wasichana wao.
Huenda kwa kuhisi hilo rais wa Seneti , David Mark, sasa amezungumza. Amewatolea wito watekaji kuawaachilia mara moja wasichana bila masharti na akasema bila shaka taifa letu liko vitani

UNAMTAZAMO GANI?

Kwani tanzania tumetoka wapi na tunakwenda wapi? nikiwa na mtazamo mpya wa sera ya serikari tatu, kwani toka miaka ya nyuma suala hili hamkuliona hadi sasa mnataka serikari tatu?kama tunavyo jua hili nisuala la kisera ambalo limeanzishwa na wapemba wanaotaka serikali tatu kwa dhumuni la haki zao za kimsingi.

swali lakujiuliza je nini kitatokea mara baada ya kuwa na serikari tatu? wa tanganyika watabaki na tanganyika yao? na wa zanzibar watabaki na zanzibar yao?pia utajiuliza tena swali kwamba neno"Zanzibar" ni muungano wa pemba na unguja  ndio uta pata zanzibar sasa pia muungano huo uta gawanyika? na  je kama watakuwa marais wa tatu je huyo rais wa muungano atachaguliwa na nani na atatokea wapi na atakaa wapi

Thursday, April 10, 2014

HABARI




Kwa nini wahutu waliwaua watutsi?

Asilimia 85 ya wananchi wa Rwanda ni wa kabila la Hutu, lakini jamii ya Tutsi imekuwa ikishikilia nyadhifa kubwa tu za ngazi za juu kwa miaka mingi.
Mwaka 1959, wahutu walimuondoa mamlakani mfalme wa Tutsi huku maelfu ya watu wa kabila hilo wakikimbilia nchi jirani kama vile Uganda.
Kikundi cha watutsi waliokuwa ukimbizini kikaunda vuguvugu waliloliita RPF ambalo lilivamia Rwanda mwaka 1990 huku vita vikiendelea hadi mwaka 1993 ambapo makubaliano ya amani yalifikiwa.
Lakini usiku wa terehe 6 Aprili mwaka1994, ndege iliyokuwa imewabeba hayati Rais Juvenal Habyarmana na mwenzake wa Burundi Cyprien Ntaryamira ilidunguliwa.
Kila mtu aliyekuwa katika ndege hiyo alifariki. RPF kilisema kuwa ndege hiyo iliangushwa na wahutu kama kisingizio cha mauaji kufanyika.
Waume waliwaua wake zao kwa hofu ya wao kuuawa

Mauaji ya Kimbari yalifanyika vipi?

Kwa mpangilio wa hali ya juu. Orodha ya majina ya waliokuwa wanapinga serikali ilitolewa kwa wapiganaji ili waweze kuwaua pamoja na familia zao.
Majirani waliuana na hata waume wa kabila ta Hutu kuwaua wake zao wa Tutsi wakisema kuwa wangeuawa ikiwa wangetaa kufanya hivyo.
Wapiganaji walitumia vitambulisho vya watu kuwaua kwani majina yao yalionyesha ikiwa walikuwa wahutu au watutsi. Maelfu ya wanawake walifugwa kama watumwa wa ngono
Jumuiya ya kimataifa ililaumiwa pakubwa kwa kutizama tu mauaji yalipokuwa yanaendelea Rwanda

Nani alijaribu kusitisha vita?

Umoja wa Mataifa na Ubelgiji zilikuwa na wanajeshi wao nchini Rwanda. Lakini umoja wa Mataifa haukuwa na idhini ya kusitisha mauaji.
Mwaka mmoja baada ya wanajeshi wa Marekani kuuawa Somalia, Marekani ilijitahidi kadri ya uwezo wake kujizuia kuingia katika vita barani Afrika.
Wanajeshi wa Ubelgiji walilazimika kuondoka nchini humo baada ya kumi kati yao kuuawa.
Walituhumiwa kwa kutofanya juhudi za kumaliza vita. Rais Paul Kagame ametuhumu Ufaransa kwa kuhusika na mauaji hao ingawa Ufaransa imekanusha vikali madai hayo.

Vita vilimalizika vipi?

Chama cha RPF kikisaidiwa na Uganda , kilianza kudhibiti sehemu kadhaa za nchi hiyo hadi Julai tarehe 4, wanajeshi wake walipoingia mjini Kigali.
Wahutu milioni mbili wengi wakiwa raia walikimbilia nchi jirani ya DRC wakihofia kushambuliwa kama hatua ya kulipiza kisasi.
Watu milioni mbili wa kabila la Hutu walikimbilia nchi jirani kuepuka kisasi cha watutsi

Vipi hali ya Rwanda sasa?

Rais Paul Kagame na chama chake RPF amesifiwa kwa kurejesha utulivu nchini Rwanda na hata kukuza uchumi wa nchi hiyo ndogo.
Pia amejaribu kuifanya Rwanda kuwa nchi inayong'aa kiteknolojia.
Lakini wakosoaji wake wanasema kuwa hapendi kukosolewa huku vifo vya wapinzani wake vikileta shaka.
Takriban watu milioni mbili walihukumiwa katika mahakama za jadi, viongozi wa mauaji wakihukumiwa katika mahakama maalum kuhusu mauaji ya Rwanda mjini Arusha Tanzania.
Kwa sasa ni hatia kwa mtu yeyote kuzungumzia ukabila nchini Rwanda, serikali inasema hii inasaidia kuzuia kutokea tena kwa mauaji kama hayo, lakini wakosoaji wa serikali wanasema hiki ni kiini macho tu kwani hisia zilizopo kuhusu ukabila huenda zikasababisha hali nyingine mbaya baadaye ikiwa watu hawatapewa uhuru wa kuzungumza.


LINI TANZANIA TUTA PANDA KIELIMU?????

Nini kinashusha viwango vya elimu TZ?


Baadhi ya mikoa Tanzania haina walimu wa kutosha
Baadhi ya watafiti wa masuala ya kielimu nchini Tanzania wamesema mgawanyo mbaya wa walimu katika ajira mpya ni moja ya mambo yanayokwamisha maendeleo ya kielimu ikiwemo kushuka viwango vya ufaulu kwa wanafunzi katika shule za msingi nchini humo.
Shirika lisilo la kiserikali la haki elimu limesema utafiti wake umebaini kuwa mikoa ya kanda ya magharibi nchini humo na ile iliyopo ziwa Victoria haijafikia malengo ya kitaifa ya idadi ya walimu katika kila shule
Katika ripoti hiyo ya utafiti wa shirika la Hakielimu, imeeleza kwamba mgawanyo wa walimu wapya haujalenga uhaba wa walimu uliopo.
Shirika hilo linasema kuwa baadhi ya mikoa iliyopokea mwalimu mmoja kwa kila wanafunzi 37, imeongezwa walimu jambo ambalo sio sawa kwa sababu baadhi ya mikoa haina walimu wa kutosha na hilo linapaswa kuzingatiwa.
Haki elimu wanasema sababu hizo ni baadhi ya mambo yanayochangia ufaulu duni , ambapo kwa kipindi cha miaka minne iliyopita ufaulu kwa shule za msingi umekuwa ni wastan wa asilimia 60 hadi 40 tu.
Limeongeza kwamba walimu wanataka kuishi katika mikoa ya karibu na hivyo kufanya kila wawezali kuwashawshi wadau kutowapeleka mikoa ya mbali.
Hata hivyo ripoti hiyo imetofautisha walimu wa sasa na wale wa miaka iliyopita. Linasema kuwa walimu wa zamani walikuwa na haiba, uzalendo na kujitolea kufanya kazi na pia walithaminiwa sana na jamii lakini leo kazi ya ualimu imekuwa kazi ya ilimradi
Baadhi ya mikoa nchini Tanzania imebuni mbinu zinazoweza kuwavutia walimu ili wafanye kazi katika maeneo yao kutokana na maeneo hayo kukosa walimu kwa miaka mingi mfululizo kutokana na mazingira duni ya kazi