Tuesday, July 15, 2014

habarika na agnes mhagama



WASANII WA SARAKASI WA ILALAMIKIA SERIKARI

Kampuni ya Simple Entertainment inayo jishughulisha na kuinua vipaji vya sarakasi  ndani ya nchi na nje ya nchi  imeiomba serikari kutupia jicho sanaa hiyo  kwani imekuwa ikisahaulika na kutothamini wa katika sanaa hiyo,licha ya kuwa imekuwa ikifanya kazi kubwa ya  mchango wa kuitambulisha nchi   na kutangaza  katika mataifa mbalimbali duniani.

Hayo yamezungumzwa hivi karibuni  na mkurugenzi wa kampuni hiyo Bwana Jacob Chinunda, wakati akizungumza na wasanii pamoja na wadau wa sanaa  katika kongamano la kila wiki la jukwaa la sanaa  linaloendeshwa na Baraza la sanaa la taifa (BASATA) jijini Dar es salaam.

Chinunda alisema sanaa ya sarakasi ina bidi ithaminiwe na kuwekewa mkazo kama sanaa nyingine , kwani ni sanaa ya kipekee ambayo imekuwa ikitambulisha nchi katika mataifa mbalimbali kupitia maonyesho ambayo wanakuwa wakifanya, kutokana na soko dogo la nchi yetu na kutothaminiwa sanaa hiyoimekuwa ikifanya na kuchezwa kila mara nje ya nchi kwa lengo la kutafuta masoko na kupendwa zaidi na watu wa nje ya nchi.

“wasanii wa sarakasi wamekuwa wakipata shida nyigi katika kupata ma agence kwani kwa nchi yetu  ni wachache sanaa ,mpaka uwe agence nilazima uwe msanii wa sarakasi,kadri siku zinavyo zidi kwenda wasanii hao wamezidi kupotea na kukatatamaa ya sanaa hiyo kulingana na changamoto wanazo kumbana nazo”alisema.

Aliongeza kwamba, sanaa hiyo imekuwa ikitambulisha vizuri jina la Tanzania  kwani kila wanapotaka kufanya  onyesho ni lazima  upeperushe bendela ya nchi yako ikiwa ni utambulisho wa sehemu uliyo toka,hali hiyo imepelekea kwa watalii wengi kupenda kuja Tanzania kwa ajili ya kujionea maonyesho hayo ya aina yake.

Licha ya hayo  alieleza changamoto wanazo kumbana nazo ikiwemo na serikali kuwasahau kwani imepelekea sanaa hiyo kuto endelea na kufahamika zaidi kimataifa na dunia nzima kama ikiwemo usumbufu mkubwa wanapokuwa wanasafiri,wanapokuwa wanataka bendera ya taifa imekuwa nitatizo kwani hadi  ina wa gharimu kutafuta vitambaa na kutengeneza bendea li iweishara ya utambulisho wan chi wanayotokea.

No comments:

Post a Comment