Sunday, July 13, 2014

SANAA YETU INAENDA WAPI



SANAA YETU INASONGA MBELE AU INAANGAMIA
Sito acha kusahau maneno ya wahenga wetu  kwani walisema  (YA KALE NIDHAHABU) wakiwa na maana  ya kituchochote cha nyuma ni bora zaidi kuliko kipya, kwani kuna watu wakiona wamepata kitu kipya basi wana dharau kitu cha nyuma.,Au kulingana na utandawazi utaona mambo yakale yakiwa mstari wa nyuma sana na kusahaurika na  kuona hayana maana  na kuendeleza  mambo ya kisasa na kusahau kabisa ubora wa mambo ya nyuma.
Msomaji wangu nazungumzia tasnia ya sanaa toka enzi za miaka ya 79 kurudi nyuma  kiukweli tamaduni za asili zilikuwa zina pamba moto na enzi hizo tulikuwa tunajivunia sanaa yetu ,sio sasa yani kadri siku zinavyoenda na pata machungu sana ninavyoona asili yetu inapotea siku hadi siku na kusahau  kabisa kama inabidi tuukuze utamaduni wetu na sio kuacha watu wakautumie utamaduni wetu.
Miaka ya nyuma tukiangalia bendi za muziki kama  sikinde,msondo,resiwanyika kweli tunaona mashairi yaliyo pangwa kwa vina na ukisikiliza unapata mafunzo mengi bila kujari unasikiliza na nani. Kiukweli miaka ya nyuma tukizungu mzia mziki tunayo ya kuzungumza lakini kwa sasa nashidwa nianzie wapi kwani kumekuwa na miziki ya aina nyingi na kila mziki una staili yake na suala la kitamatuni au maadili halija wekewa mkazo sana na kudharaulika kabisa.
Nikiangalia hali ya sanaa ya sasa naona itakuja kufika sehemu suala la utamaduni likapotea kabisa kwani kwa sasa kila mtu anajaribu kufanya mziki kulingana nay eye anataka nini na si kuangalia je niwatu gani watakwenda kusikiliza au kuangalia kazi yangu , jambo hilo linasikitisha sana kwani kuna baadhi ya nyimbo na video za muziki zinapotosha kabisa ukiangalia kama mtu mzima umekaa na watoto itabidi usimame na kutoka nje je/ halihiyo inapeleka wapi tamaduni  yetu. Ni tuna kuza au kubomoa?
Kama wasanii ina bidi tufike mahari na kubadilika na kujalibu kuangalia wapi tuliko toka na wapi tunaenda ili kuhakikisha kazi zetu zinafika sehemu nzuli na kuweza kufahamika mataifa na mataifa ,lakini kama utaendeleza kuharibu kwa kufanya sanaa za ajabu kama ngoma za vigodoro, ngoma za kanga moja  na nyingine zinazo vunja utamaduni hatuta songa mbele na tutaibua tamaduni nyingine ni mhimu kutunza tamaduni zetu. Msomaji kwaleo ni hayo tuu panapo majariwa tutaendelea

No comments:

Post a Comment