Thursday, May 21, 2020

FAHAMU JINSI YA KUMDATISHA MPENZI WAKO KWA KUZUNGUMZA NAE







Unavyozungumza na mpenzi wako ni tofauti kabisa na unavyozungumza na watu wengine. Ni hatari sana kutumia lugha ya ukali ama isiyo ya kiungwana kwa mpenzi wako.
Unatakiwa kufahamu kwamba, mpenzi wako ni mtu muhimu sana katika maisha yako hivyo unatakiwa kuwa makini pindi unapozungumza naye.

Kuonesha kwamba wapo wasiojua mapenzi ni nini, unamkuta mtu anamwita mpenzi wake majina kama vile mshamba, demu, shembe na mengine mengine kama hayo. Mpenzi wako kweli umuite demu? Na wale wengine kule mtaani utawaita nani?

Huo si ustaarabu na kamwe mapenzi yenu hayawezi kushamiri kwa mtindo huo. Kuna wengine matusi hayawaishi midomoni mwao. Kwa kufanya hivyo jua tu kwamba unamboa laazizi wako.
Aidha mapozi katika uzungumzaji wako ni miongoni mwa vitu vinavyoweza kumdatisha mpenzi wako. Ukiwa na mpenzi wako usiongee kama chiriku au kama unagombana na mtu. Ongea kwa mapozi na hilo litamfanya akutofautishe wewe na watu wengine.

Kuna ambao wanapozungumza na wapenzi wao hawapitishi sentensi bila kutaja neno Dear ama Sweet. Hakika inavutia na ni mbolea tosha katika penzi la watu hao.
Lakini pia kuna baadhi ya maneno ambayo ukiyafanya kuwa sehemu ya maisha yako yanaweza kumvutia mpenzi wako. Kwa mfano neno NAKUPENDA!

Hakuna asiyefurahia kupendwa hata kama ni mtoto mdogo, anafurahi sana kusikia neno 'Nakupenda' kutoka kwa watu wake wa karibu. Lakini linapokuja suala la mahusiano ya kimapenzi, neno hilo linachukua nafasi kubwa sana.

Ili kulifanya neno hilo kuwa na uzito wengine hulitamka kwa lugha ya kigeni yaani 'I love you Dear au sweet', ni sawa tu kwani maana ni ile ile. Huo ni mfano wa maneno ambayo ni chachu katika mapenzi.
Pia unatakiwa kuwa mwepesi wa kushukuru. Wengine hata wapenzi wao wajitahidi kuwafanyia mambo mazuri vipi, lakini ni wagumu sana kutamka neno ASANTE.

Hata wanapowakosea wapenzi wao ni wagumu sana kuomba samahani. Kwa taarifa yako kama wewe ni mmoja wa wenye tabia hiyo elewa kwamba unamboa sana mpenzi wako.
Pia mnapokuwa faragha na mpenzi mkistarehe,baada ya kukufanyia kile ambacho roho yako imefurahi, mwambie asante kwa kukupeleka kwenye sayari mpya ya mahaba.

TABIA ZAKO
Huu ndio msingi imara wa uhusiano wa kimapenzi. Wapo wanawake ambao ni wazuri na wenye kila sifa ya kuwa na wapenzi bora, lakini kutokanana tabia zao chafu wamekuwa wakiachwa kila wanapoingia katika uhusiano.

Nani atakupenda na kudiriki kuendelea kuwa katika uhusiano na wewe kama tabia zako si nzuri? Wengi wetu tunapenda kupata sifa ya kuwapata wapenzi ama wachumba wenye tabia nzuri ili tuweze kusifiwa na marafiki zetu pamoja na wazazi.

Kwa maana hiyo basi, kuwa makini sana na tabia ambazo unajua haziwezi kumvutia mpenzi wako ama jamii inayowazunguka kama vile WIVU uliopitiliza kiasi cha kuwa kero, kutaka makuu pamoja na tamaa zisizo na msingi.

Nimeweka wivu juu kutokana na ukweli kwamba, kuna wanawake hata wakiwakuta wapenzi wamesimama ama kupigiwa simu na mtu wa jinsia tofauti bila kujua ukweli wa mambo wanaanzisha vurumai, huu ni ulimbukeni.

JINSI UNAVYOMRIDHISHA
Yote hayo hapo juu ni tisa, lakini kumi ni jinsi unavyoweza kumridhisha mpenzi wako hasa mnapokuwa faragha mkipeana raha za dunia.

Hata kama una tabia nzuri na umbile la kumvutia kiasi gani, kama huna utaalam na ujuzi wa kutosha katika kumpa raha mpenzi wako hasa linapokuja suala la tendo la ndoa, lazima penzi ama ndoa yako itakuwa na walakini.

Nilishawahi kusema huko nyuma kwamba, tunapozungumzia mapenzi hatumaanishi ngono. Ngono ama tendo la ndoa ni sehemu tu ya mapenzi ambayo haichukui nafasi kubwa sana kama baadhi yetu tunavyochukulia.

Lakini kitu ambacho kimekuwa kikiwavutia walio wengi waume kwa wanawake ni utundu na ubunifu wakati mnapokuwa faragha. Kinachotakiwa ni kupeana kile roho inataka ili suala la kusalitiana lisiwepo.










DAWA YA MALARIA JE INATIBU CORONA?

Jaribio la matumizi ya dawa za malaria kuona kama zinaweza kuzuia ugonjwa wa Corona limeanza nchini Uingereza katika mji wa Brighton na Oxford.
Chloroquine, hydroxychloroquine au placebo zitatolewa kwa wafanyakazi wa afya zaidi ya 40,000 kutoka Ulaya, Afrika, Asia na Amerika ya kusini.
Washiriki wote ni watumishi wa afya ambao wanahudumia wagonjwa wa Covid-19.
Rais Donald Trump alikosolewa baada ya kusema kuwa ametumia dawa ya malaria iitwayo hydroxychloroquine, licha ya angalizo kuwa inawezekana si salama kutumia dawa hiyo kwa ajili ya corona.
Mshiriki wa kwanza, Uingereza katika jaribio la kwanza la kimataifa imesema siku ya Alhamisi katika hospitali ya Brighton na hospitali ya chuo kikuu cha Sussex pamoja na hospitali ya John Radcliffe mjini Oxford.
Watapewa dawa ya hydroxychloroquine au placebo kwa kipindi cha miezi mitatu.
Wakati Asia, washiriki watapewa chloroquine au placebo.
Mipango ya awali ni katika majimbo 25 ya Uingereza na matokeo yanatarajiwa mwishoni mwa mwaka.
Jaribio hilo liko wazi kwa yeyote ambaye anatoa huduma moja kwa moja kwa wagonjwa wenye virusi vya corona nchini Uingereza, ikiwa kama bado hawajapata maambukizi ya virusi vya corona.
Jaribio hili litaangalia kama dawa hizo zitaweza kuzuia wafanyakazi wa afya kupata maambukizi ya virusi vya corona kutoka kwa wagonjwa.

'Ina manufaa au ni hatari'

Utafiti mmoja wa Prof Nicholas White kutoka chuo kikuu cha Oxford alisema: "Kiukweli hatufahamu bado kama chloroquine au hydroxychloroquine kama ni kinga au zina madhara dhidi ya Covid-19."
Lakini alisema, utafiti wa maeneo mbalimbali kama huu , ambapo si mshiriki au mtafiti anafahamu kuwa kupewa dawa hiyo ndio namna nzuri ya kujua umuhimu wa dawa husika.
"Chanjo ambayo ni salama na yenye uhakika itachukua muda mrefu kupatikana," alisema Prof Martin Llewelyn kutoka Brighton na chuo cha afya cha Sussex, ambaye pia anaongoza utafiti huo.
"Kama dawa za malaria za chloroquine na hydroxychloroquine zinaweza ,kupunguza urahisi wa mtu kuambukizwa virusi vya corona, basi itakuwa jambo bora zaidi ambalo litasaidia."
Dawa hizo zinaweza kupunguza homa na maambukizi na kuweza kutumika pia kwa ajili ya kuzuia na kutibu malaria.
US President Donald Trump speaking at the White HouseHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionRais Trump alizungumzia kabla kuhusu matumizi ya dawa hizi kwa ajili ya Covid-19
Kituo cha kujitolea cha Lupus nchini Uingereza na Marekani kimetoa wasiwasi wake kuhusu ongezeko la uhitaji wa dawa hiyo kwa ajili ya virusi vya corona kunaweza kuhatarisha hali za wagonjwa ambao wanazitegemea tayari, kama zitapungua wagonjwa wa malaria watapata shida kuzipata ili kutibiwa.
Dawa hizo zimepata umaarufu baada ya rais wa Marekani Donald Trump kusema kuwa dawa hizo zinaweza zikasaidia katika janga hili la corona, na wiki hii alitumia dawa ya hydroxychloroquine ili kujizuia kupata maambukizi ya corona.
Mamlaka ya dawa na chakula nchini Marekani ilitoa angalizo dhidi ya matumizi ya dawa hizo nje ya hospitali, wakati wakitoa ruhusa ya dawa hizo kutumika katika kesi kadhaa au majaribio ya kitabibu.
Wakati chuo kikuu cha Oxford kikifanya jaribio la kuzuia maambukizi katika mazingira ya huduma za afya, shirika la afya duniani limetoa angalizo kuwa baadhi ya watu ambao wanajitibu wenyewe wanaweza kupata madhara makubwa.
Hazijaonekana kuwa salama na zenye uhakika wa kuzuia maambukizi ya virusi vya corona bali kuna hatari ya kupata matatizo makubwa ya moyo.
Utafiti huo umejumuisha watafiti kutoka Uingereza, Thailand, Vietnam, Laos, Cambodia na Italia.


Wednesday, May 20, 2020

MUNGU ASIKIA MAOMBI YA WATANZANIA JUU YA COVID 19

Rais Magufuli akiwa safarini kutokea Chato  alisimama mkoani Singida kuwasalimia wananchi na kuzungumza machache yakiwemo kuhusu kutakuwa na siku tatu za kumshukuru Mungu kwa Maajabu ya kutuepusha na Corona.