Saturday, July 16, 2016

LEO WATANZANIA MACHO YOTE KWA YANGA

TIMU ya Yanga leo inatupa karata yake muhimu katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuwakaribisha Medeama FC ya Ghana, mchezo utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga inayoshika mkia kwenye kundi lake la A, na inahitaji ushindi katika mchezo wa leo ili kurudisha matumaini ya kucheza nusu fainali ya michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa upande wa klabu barani Afika.
Kocha wa Yanga, Hans Pluijm amesema jeshi lake lipo tayari kwa ajili ya mchezo huo huku akijivunia kurejea kwa mshambuliaji wake Amissi Tambwe, aliyeukosa mchezo uliopita kutokana na kuwa na kadi mbili za njano alizozipata kwenye michezo iliyopita.
Uwepo wa Tambwe ni wazi utaongeza ukali wa safu ya ushambuliaji, ambayo haijafunga hata bao moja katika mechi mbili zilizopita ambazo zote wamepoteza mbele ya MO Bejaia na TP Mazembe na kuifanya timu hiyo iburuze mkia kwenye kundi lake.
Pluijm alisema amekiandaa kikosi chake kucheza kwa kushambulia zaidi ili kuhakikisha wanapata mabao mawili ya haraka kwenye kipindi cha kwanza ili kuwavunja nguvu wapinzani wao Medeama ambao wamekuja nchini wakiwa na matumaini ya kuvuna pointi tatu.
Mholanzi huyo alisema anataka kuiona timu yake ikicheza eneo la wapinzani wao kwa sehemu kubwa ya mchezo jambo ambalo litawarahisishia kupata bao muda wowote hasa kutokana na mpango wa kutumia washambuliaji watatu kwenye mchezo huo.
“Ukweli huu ni mchezo muhimu kwetu lazima tushinde ili ndoto zetu za kucheza nusu fainali ziweze kutimia ndiyo sababu tumejipanga vizuri katika muda tulioupata baada ya kucheza na TP Mazembe na ninafurahi kuona wachezaji wangu wote wapo katika hali nzuri na wanajua umuhimu wa ushindi katika mchezo huo,”alisema Pluijm.
Pluijm alisema anajua mchezo utakuwa mgumu kutokana na Medeama nao kuhitaji ushindi, lakini atahakikisha wanaitumia vizuri nafasi ya kucheza nyumbani kupata ushindi ili pia kuwafurahisha mashabiki wao ambao waliwaangusha katika mchezo uliopita kwa kufungwa na TP Mazembe.
Alisema baada ya kupoteza michezo miwili iliyopita wasingependa kupata matokeo hayo kwa sababu mipango yao ni kuhakikisha wanaanza kushinda mchezo huo na mingine iliyobaki ili kutimiza kile walichokipanga.
Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro', anatarajiwa kuanza kwenye mchezo huo akiziba nafasi ya Kelvin Yonda ambaye hatocheza mechi hiyo kutokana na kuwa na kadi mbili za njano, lakini pia kiungo Deusi Kaseke huenda asicheze kutokana na kuwa majeruhi baada ya kupata ajali ya piki piki siku za karibuni.
Kocha wa Medeama Prince Yaw Owusu, ametamba kuwa amekuja Tanzania kuchukua pointi tatu ili waweze kufufa matumaini ya kucheza hatua ya nusu fainali. Owusu, alisema anawajua vizuri wenyeji wao Yanga, na haoni kitu ambacho kinaweza kumzuia asipate ushindi kutokana na kikosi chake kuwa katika kiwango cha juu hivi sasa baada ya kufanya vizuri kwenye mechi za ligi ya Ghana.
“Najua mchezo utakuwa mgumu lakini kuijua kwangu Yanga kutasaidia kupunguza presha kwa wachezaji wangu ambao naamini hakuna anayeijua Tanzania wala Yanga yenyewe, lakini tumekuja tukihitaji pointi tatu na nina hakika wa kuzipata kwa sababu katika timu nyepesi kwenye kundi letu basi ni hii,”alisema kocha huyo.
Owusu alisema kikosi chake kitaingia uwanjani kikiwa kinawategemea zaidi viungo wa

Monday, June 20, 2016

Nape aongoza mamia kufanya Yoga

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye jana aliongoza mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam katika maadhimisho wa Siku ya Yoga Duniani kwa kushiriki kikamilifu kufanya mazoezi.
Nape aliwasili katika ufukwe wa Coco, ambapo maadhimisho hayo yalikuwa yakifanyika jana asubuhi na baada ya kuhutubia alitumia dakika kadhaa kufanya mazoezi hayo. Alikuwa na Balozi wa India nchini Sandeep Arya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambapo walipewa wasaa wao peke yao kwanza kufanya mazoezi hayo.
Baada ya hapo ilifika zamu ya watu wote waliokuwa viwanjani hapo kufanya mazoezi, ambapo pia Nape akiwa na Makonda, Balozi wa India hapa nchini pamoja na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Peter Kallaghe na wakazi wengine kuanza mazoezi hayo. Nape ambaye awali alisema kuwa alipokuwa akisoma nchini India alijifunza kwa ukaribu zaidi Yoga alionesha uwezo mkubwa wa kumudu mazoezi hayo.
Tukio hilo lililodumu kwa takribani dakika 35, ambapo waziri huyo pamoja na wenzake walifanya mazoezi hayo kwa umakini bila ya kupumzika. Walifanya mazoezi ya kunyonga miguu, kiuno, mgongo, mbavu, shingo pamoja na mazoezi mengine kama kuvuta pumzi kwa kutumia tundu moja la pua, mdomo na pamoja na mbinu nyingine za kuimarisha pumzi.
Kisha lilifuata zoezi la kunyanyua miguu juu, kufunga macho kisha kumalizia na kuomba. Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilika kwa maadhimisho hayo, Nape alisema kuwa wizara yake itahakikisha kuwa inabainisha aina ya tamaduni zenye asili ya mazoezi ndani yake na kuziendeleza.
Alisema kuwa Yoga ilianza kama utamaduni wa India, ambapo kwa sasa umekuwa ni utamaduni mkubwa duniani na umekuwa ukiadhimishwa katika kila nchi zenye ubalozi wa India. Alisema kwa kuwa Yoga inalenga kuwaweka pamoja wananchi bila ya kujali tofauti zao za kidini, kabila, uraia hata jinsia, inaendana moja kwa moja na sera ya Tanzania.
“Yoga ni moja kati ya aina bora ya mazoezi ya kufanya ambapo inasaidia kuimarisha kila kona ya mwili, na mimi nimejifunza mengi kuhusiana na Yoga wakati nikiwa India ninasoma na leo nimejikumbushia mengi sana,” alisema Nape.
Kwa upande wake Balozi wa India hapa nchini, Sandeep Arya alionesha kufurahishwa na idadi ya wananchi waliojitokeza katika ufukwe huo na kuwataka kuendelea kujitokeza kwa wingi zaidi katika kituo cha Utamaduni cha India hapa nchini kinachotoa mafunzo hayo.
Alisema kuwa Yoga ni zaidi ya mazoezi kwa kuwa yanasaidia pia kuondoa msongo wa mawazo, kukuza namna ya kufikiria mambo na pia ni njia mojawapo ya tiba kwa baadhi ya magonjwa.
“Sisi India Yoga ni utamaduni na tena ni njia mojawapo ya kujiimarisha zaidi katika maisha ya kila siku kwa kuwa kwanza ni nidhamu na pia ni mfumo wa maisha ya kila siku tunayoishi kuanzia kula na mengineyo,” alisema balozi huyo.
Aliongeza: “Kwa hapa nchini kupitia kituo cha utamaduni kilichopo chini ya Ubalozi wa India, tunatoa mafunzo kwa kila atakaye kujifunza Yoga na watu wafike kufundishwa zaidi”.
Kwa upande wake, Makonda alitoa wito wa matumizi ya lugha ya Kiswahili pia katika utoaji wa mafunzo hayo ili kila mtu aweze kuelewa kirahisi zaidi mazoezi hayo kitu ambacho kilifanyika hapo Coco ambapo mbunifu wa mavazi nchini Ally Remtulah alikuwa akitafsiri maelekezo yaliyokuwa yakitolewa na wataalamu wa Yoga kwa lugha ya Kiingereza na kuzungumza Kiswahili.
Mchezo huo umeonekana kupendwa na wengi na hata wale ambao bado hawajajiunga wameonesha nia ya kutaka kujiunga na huenda wengi wakajitokeza katika kituo hicho cha India kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo. Pia mchezo huo unaweza kumsaidia mtu kujiamini mbele ya maadui pale anaposhambuliwa na majambazi, waporaji au vibaka.

Simba wamshindwa Okwi

MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili wa klabu ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amesema hawana mpango wa kumsajili kwa mara nyingine mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda Emmanuel Okwi, kwa sababu tayari kuna wachezaji wanafanya mazungumzo nao kutoka Ivory Coast na Zimbabwe.
Hans Poppe, alisema Okwi ni rafiki yao mkubwa na anakubali uwezo wake, lakini mazingira ya kumsajili kutoka kwenye klabu yake anayoichezea hivi sasa ya Sonderjyske ya Denmark ni magumu ndiyo maana wameona kuachana naye na kutafuta wachezaji wengine ambao wapo huru na wale wa bei nafuu.
“Okwi ni mchezaji mzuri lakini kwa bajeti yetu hatutaweza kumsajili kwa sababu pesa ambazo tungemsajili yeye kutoka Denmark tuna uwezo wa kupata wachezaji wazuri tena zaidi yake kutoka mataifa ya Ivory Coast, Zimbabwe na kwingineko Afrika,” alisema Hans Poppe.
Kiongozi huyo alisema pamoja na Mganda huyo, kuichezea kwa mafanikio timu yao na kuwa na mapenzi makubwa na Simba, lakini wameona ni vyema wakaliweka swala lake pembeni huku wakipambana kutafuta wachezaji wengine ambao itakuwa ni mara ya kwanza kucheza Ligi ya Tanzania na wanahitaji kupata mafanikio ili kujenga majina yao.
Alisema wao kama viongozi wamekubaliana wasisajili wachezaji kutoka mataifa ya Uganda na Kenya kutokana na usumbufu wanaoupata mara kwa mara na hiyo ni sababu nyingine inayowafanya kuliweka pembeni jina la Okwi kwa sababu msimu ujao wamepania kurudisha heshima yao na siyo malumbano na wachezaji.
“Msimu uliopita tulikuwa na wachezaji watatu kutoka Uganda, tuliona shida yake kitu ambacho naweza kusema kimechangia kututoa kwenye mbio za ubingwa, tumejifunza na tusingependa mambo kama hayo yakajitokeza tena kwenye timu yetu ndiyo maana tumeona safari hii tubadili twende mataifa mengine yaliyopiga hatua zaidi kisoka,” alisema.
Okwi anatajwa kutaka kurudi kwenye klabu ya Simba tena hata kwa mkopo baada ya kukosa furaha kwenye klabu hiyo ya Sonderjyske, ambako ameshindwa kuwika kama ilivyokuwa Simba ambapo aliweza kupataji jina kubwa na kujizolea umaarufu wa hali ya juu na kuwa kipenzi cha wana Msimbazi.

Je unajua??

Kuwa wakwanza kuwafurahisha wakupigiao kwa kusikia muito wa jina lako pindi wakupigiapo..
Nirahisi sana unachotakiwa kufanya nikubonyeza * 148*01*4*2| alama ya reli..
Utachagua nametune kujiunga ..ukifuatia na jina lako.. kuanzia hapo marafiki zako watasikia maana ya jina lako pindi wa kupigiapo.. jaribu sasa.