Thursday, July 24, 2014

JE WA SANII WANAJUA UMUHIMU WA BIMAA?


MANUFAA YA BIMA KWA WASANII

Na AGNES MHAGAMA

  Kwakupitia  programu  ya  kila wiki  Baraza la sanaa (BASATA)  limetoa  elimu  kwa wadau wa sanaa  na wasanii  kuhusu  umuhimu wa kuwa na bima kwa  ajiri  ya ulinzi wa afya zao pamoja na mali zao.

Hayo  yamebainishwa na Afisa  masoko   wa kampuni ya MGEN  inayojishughulisha na mambo ya bima na Bw.JAFARRY JUMBE wakati akiongea na wasanii pamoja na wadau wa sanaa katika  Jukwaa la  sanaa  jijini Dar es salaam.

Bw.jumbe alisema  wasanii watafaidika  na huduma hiyo popote watakapo kama vile,msanii akipata matatizo ya ajali, kuungua kwa mali zake, kupatwa na maradhi    , kama kampuni ya MGEN  itahusika na ulipaji wote wa awali  wa mali yake.

Aliongeza kwamba, msanii kuwa na bima ni mhimu kwani katika kazi zake za kukuza sanaa anakumbana na changamoto mbalimbali kwahiyo  kama atakuwa na Bima ita msaidia yeye kuweza kufidia baadhi ya sehemu atakazo kuwa ameshindwa kutekeleza.
Hatahivyo alisema kampuni imeamua  kugawa bima kwa ngazi mbalimbali  ilikulahisisha kila mtu aweze kuwa na bima mojawapo  kama  bima ya mtu mmoja, bima ya vikunndi vya watu ,bima ya mali ,ili  kumsaidia msanii aweze kuwa na bima itakayo msaidia katika ulinzi wa mali zake kwa haraka zaidi.

Licha ya hayo aliwataka wasanii kutokuwa na hofu ya gharama  na kuepuka maneno ya mitaani yanayo  toa taarifa za uongo juu ya  huduma hiyo kwani kampuni hiyo imeweza kuweka gharama ndogo zitakazo mfanya mtu yoyote aweze kukidhi.




                            

No comments:

Post a Comment