Fainali na Real ni Chelsea au Atletico?
Nahodha wa Chelsea John Terry na Eden Hazard watakuwa tayari
katika kikosi cha Jose Mourinho kitakachocheza dhidi ya Atletico Madrid katika
mchezo wa marudiano hatua ya nusu fainali ya Kombe la UEFA mjini London,
Jumatano.
Hata hivyo mlinda mlango tegemeo wa Chelsea, Petr Cech hatajumuishwa kwenye
kikosi hicho kutokana na kuwa majeruhi.Nahodha wa Atletico Gabi anatumikia adhabu ya kadi, ambapo mchezaji kiungo wa zamani wa Chelsea Tiago Mendes anatarajiwa kuchukua nafasi yake.
Swali linalobaki ni nani kati ya Chelsea na Atletico atakayeungana na Real Madrid kucheza fainali ya UEFA mwaka 2014 mjini Lisbon? Real imefuzu kucheza fainali za UEFA mwaka huu baada ya kuisambaratisha Bayern Munich kwa jumla ya mabao 5-0 na hivyo kuivua rasmi ubingwa na kuliacha kombe hilo likiwaniwa na timu mpya.
No comments:
Post a Comment