Nini kinashusha viwango vya elimu TZ?
Baadhi ya watafiti wa masuala ya
kielimu nchini Tanzania wamesema mgawanyo mbaya wa walimu katika ajira
mpya ni moja ya mambo yanayokwamisha maendeleo ya kielimu ikiwemo
kushuka viwango vya ufaulu kwa wanafunzi katika shule za msingi nchini
humo.
Shirika lisilo la kiserikali la haki elimu
limesema utafiti wake umebaini kuwa mikoa ya kanda ya magharibi nchini
humo na ile iliyopo ziwa Victoria haijafikia malengo ya kitaifa ya idadi
ya walimu katika kila shuleKatika ripoti hiyo ya utafiti wa shirika la Hakielimu, imeeleza kwamba mgawanyo wa walimu wapya haujalenga uhaba wa walimu uliopo.
Shirika hilo linasema kuwa baadhi ya mikoa iliyopokea mwalimu mmoja kwa kila wanafunzi 37, imeongezwa walimu jambo ambalo sio sawa kwa sababu baadhi ya mikoa haina walimu wa kutosha na hilo linapaswa kuzingatiwa.
Haki elimu wanasema sababu hizo ni baadhi ya mambo yanayochangia ufaulu duni , ambapo kwa kipindi cha miaka minne iliyopita ufaulu kwa shule za msingi umekuwa ni wastan wa asilimia 60 hadi 40 tu.
Limeongeza kwamba walimu wanataka kuishi katika mikoa ya karibu na hivyo kufanya kila wawezali kuwashawshi wadau kutowapeleka mikoa ya mbali.
Hata hivyo ripoti hiyo imetofautisha walimu wa sasa na wale wa miaka iliyopita. Linasema kuwa walimu wa zamani walikuwa na haiba, uzalendo na kujitolea kufanya kazi na pia walithaminiwa sana na jamii lakini leo kazi ya ualimu imekuwa kazi ya ilimradi
Baadhi ya mikoa nchini Tanzania imebuni mbinu zinazoweza kuwavutia walimu ili wafanye kazi katika maeneo yao kutokana na maeneo hayo kukosa walimu kwa miaka mingi mfululizo kutokana na mazingira duni ya kazi
No comments:
Post a Comment