Tuesday, March 11, 2014

Kutana na Daniel Kish: Kipofu aliyejifunza kuona kwa kutumia Sauti.


daniel kish kipofu anayeona

Daniel Kish alipoteza uwezo wake wa kuona tangu akiwa na umri wa miezi 13, kwa ugonjwa wa Saratani.
Kwa kutumia sauti (Clicking Sound)  inayoitoa kwa kugonga ulimi wake kwenye kuta za midomo na kufuatilia Mwangwi wake, Kish anaweza kutambua vitu vyote vilivyo karibu yake. Kish hutumia ujuzi huo ujulikanao kama Echolocation, ambao pia hutumiwa na mnyama Popo “Kuona” na kujua vitu vinavyo mzunguka.
Kwa kutumia ujuzi huo Kish anauwezo wa kundesha baiskeli kwenye barabara za kawaida. Pia anauwezo wa kutambua majengo yaliopo umbali hadi mita 300, kutofautisha aina ya magari na mambo mengine yanayo mwezesha kuishi maisha yake kama mtu anayeona.
Maoni yako

No comments:

Post a Comment