Thursday, May 21, 2020

FAHAMU JINSI YA KUMDATISHA MPENZI WAKO KWA KUZUNGUMZA NAE







Unavyozungumza na mpenzi wako ni tofauti kabisa na unavyozungumza na watu wengine. Ni hatari sana kutumia lugha ya ukali ama isiyo ya kiungwana kwa mpenzi wako.
Unatakiwa kufahamu kwamba, mpenzi wako ni mtu muhimu sana katika maisha yako hivyo unatakiwa kuwa makini pindi unapozungumza naye.

Kuonesha kwamba wapo wasiojua mapenzi ni nini, unamkuta mtu anamwita mpenzi wake majina kama vile mshamba, demu, shembe na mengine mengine kama hayo. Mpenzi wako kweli umuite demu? Na wale wengine kule mtaani utawaita nani?

Huo si ustaarabu na kamwe mapenzi yenu hayawezi kushamiri kwa mtindo huo. Kuna wengine matusi hayawaishi midomoni mwao. Kwa kufanya hivyo jua tu kwamba unamboa laazizi wako.
Aidha mapozi katika uzungumzaji wako ni miongoni mwa vitu vinavyoweza kumdatisha mpenzi wako. Ukiwa na mpenzi wako usiongee kama chiriku au kama unagombana na mtu. Ongea kwa mapozi na hilo litamfanya akutofautishe wewe na watu wengine.

Kuna ambao wanapozungumza na wapenzi wao hawapitishi sentensi bila kutaja neno Dear ama Sweet. Hakika inavutia na ni mbolea tosha katika penzi la watu hao.
Lakini pia kuna baadhi ya maneno ambayo ukiyafanya kuwa sehemu ya maisha yako yanaweza kumvutia mpenzi wako. Kwa mfano neno NAKUPENDA!

Hakuna asiyefurahia kupendwa hata kama ni mtoto mdogo, anafurahi sana kusikia neno 'Nakupenda' kutoka kwa watu wake wa karibu. Lakini linapokuja suala la mahusiano ya kimapenzi, neno hilo linachukua nafasi kubwa sana.

Ili kulifanya neno hilo kuwa na uzito wengine hulitamka kwa lugha ya kigeni yaani 'I love you Dear au sweet', ni sawa tu kwani maana ni ile ile. Huo ni mfano wa maneno ambayo ni chachu katika mapenzi.
Pia unatakiwa kuwa mwepesi wa kushukuru. Wengine hata wapenzi wao wajitahidi kuwafanyia mambo mazuri vipi, lakini ni wagumu sana kutamka neno ASANTE.

Hata wanapowakosea wapenzi wao ni wagumu sana kuomba samahani. Kwa taarifa yako kama wewe ni mmoja wa wenye tabia hiyo elewa kwamba unamboa sana mpenzi wako.
Pia mnapokuwa faragha na mpenzi mkistarehe,baada ya kukufanyia kile ambacho roho yako imefurahi, mwambie asante kwa kukupeleka kwenye sayari mpya ya mahaba.

TABIA ZAKO
Huu ndio msingi imara wa uhusiano wa kimapenzi. Wapo wanawake ambao ni wazuri na wenye kila sifa ya kuwa na wapenzi bora, lakini kutokanana tabia zao chafu wamekuwa wakiachwa kila wanapoingia katika uhusiano.

Nani atakupenda na kudiriki kuendelea kuwa katika uhusiano na wewe kama tabia zako si nzuri? Wengi wetu tunapenda kupata sifa ya kuwapata wapenzi ama wachumba wenye tabia nzuri ili tuweze kusifiwa na marafiki zetu pamoja na wazazi.

Kwa maana hiyo basi, kuwa makini sana na tabia ambazo unajua haziwezi kumvutia mpenzi wako ama jamii inayowazunguka kama vile WIVU uliopitiliza kiasi cha kuwa kero, kutaka makuu pamoja na tamaa zisizo na msingi.

Nimeweka wivu juu kutokana na ukweli kwamba, kuna wanawake hata wakiwakuta wapenzi wamesimama ama kupigiwa simu na mtu wa jinsia tofauti bila kujua ukweli wa mambo wanaanzisha vurumai, huu ni ulimbukeni.

JINSI UNAVYOMRIDHISHA
Yote hayo hapo juu ni tisa, lakini kumi ni jinsi unavyoweza kumridhisha mpenzi wako hasa mnapokuwa faragha mkipeana raha za dunia.

Hata kama una tabia nzuri na umbile la kumvutia kiasi gani, kama huna utaalam na ujuzi wa kutosha katika kumpa raha mpenzi wako hasa linapokuja suala la tendo la ndoa, lazima penzi ama ndoa yako itakuwa na walakini.

Nilishawahi kusema huko nyuma kwamba, tunapozungumzia mapenzi hatumaanishi ngono. Ngono ama tendo la ndoa ni sehemu tu ya mapenzi ambayo haichukui nafasi kubwa sana kama baadhi yetu tunavyochukulia.

Lakini kitu ambacho kimekuwa kikiwavutia walio wengi waume kwa wanawake ni utundu na ubunifu wakati mnapokuwa faragha. Kinachotakiwa ni kupeana kile roho inataka ili suala la kusalitiana lisiwepo.










DAWA YA MALARIA JE INATIBU CORONA?

Jaribio la matumizi ya dawa za malaria kuona kama zinaweza kuzuia ugonjwa wa Corona limeanza nchini Uingereza katika mji wa Brighton na Oxford.
Chloroquine, hydroxychloroquine au placebo zitatolewa kwa wafanyakazi wa afya zaidi ya 40,000 kutoka Ulaya, Afrika, Asia na Amerika ya kusini.
Washiriki wote ni watumishi wa afya ambao wanahudumia wagonjwa wa Covid-19.
Rais Donald Trump alikosolewa baada ya kusema kuwa ametumia dawa ya malaria iitwayo hydroxychloroquine, licha ya angalizo kuwa inawezekana si salama kutumia dawa hiyo kwa ajili ya corona.
Mshiriki wa kwanza, Uingereza katika jaribio la kwanza la kimataifa imesema siku ya Alhamisi katika hospitali ya Brighton na hospitali ya chuo kikuu cha Sussex pamoja na hospitali ya John Radcliffe mjini Oxford.
Watapewa dawa ya hydroxychloroquine au placebo kwa kipindi cha miezi mitatu.
Wakati Asia, washiriki watapewa chloroquine au placebo.
Mipango ya awali ni katika majimbo 25 ya Uingereza na matokeo yanatarajiwa mwishoni mwa mwaka.
Jaribio hilo liko wazi kwa yeyote ambaye anatoa huduma moja kwa moja kwa wagonjwa wenye virusi vya corona nchini Uingereza, ikiwa kama bado hawajapata maambukizi ya virusi vya corona.
Jaribio hili litaangalia kama dawa hizo zitaweza kuzuia wafanyakazi wa afya kupata maambukizi ya virusi vya corona kutoka kwa wagonjwa.

'Ina manufaa au ni hatari'

Utafiti mmoja wa Prof Nicholas White kutoka chuo kikuu cha Oxford alisema: "Kiukweli hatufahamu bado kama chloroquine au hydroxychloroquine kama ni kinga au zina madhara dhidi ya Covid-19."
Lakini alisema, utafiti wa maeneo mbalimbali kama huu , ambapo si mshiriki au mtafiti anafahamu kuwa kupewa dawa hiyo ndio namna nzuri ya kujua umuhimu wa dawa husika.
"Chanjo ambayo ni salama na yenye uhakika itachukua muda mrefu kupatikana," alisema Prof Martin Llewelyn kutoka Brighton na chuo cha afya cha Sussex, ambaye pia anaongoza utafiti huo.
"Kama dawa za malaria za chloroquine na hydroxychloroquine zinaweza ,kupunguza urahisi wa mtu kuambukizwa virusi vya corona, basi itakuwa jambo bora zaidi ambalo litasaidia."
Dawa hizo zinaweza kupunguza homa na maambukizi na kuweza kutumika pia kwa ajili ya kuzuia na kutibu malaria.
US President Donald Trump speaking at the White HouseHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionRais Trump alizungumzia kabla kuhusu matumizi ya dawa hizi kwa ajili ya Covid-19
Kituo cha kujitolea cha Lupus nchini Uingereza na Marekani kimetoa wasiwasi wake kuhusu ongezeko la uhitaji wa dawa hiyo kwa ajili ya virusi vya corona kunaweza kuhatarisha hali za wagonjwa ambao wanazitegemea tayari, kama zitapungua wagonjwa wa malaria watapata shida kuzipata ili kutibiwa.
Dawa hizo zimepata umaarufu baada ya rais wa Marekani Donald Trump kusema kuwa dawa hizo zinaweza zikasaidia katika janga hili la corona, na wiki hii alitumia dawa ya hydroxychloroquine ili kujizuia kupata maambukizi ya corona.
Mamlaka ya dawa na chakula nchini Marekani ilitoa angalizo dhidi ya matumizi ya dawa hizo nje ya hospitali, wakati wakitoa ruhusa ya dawa hizo kutumika katika kesi kadhaa au majaribio ya kitabibu.
Wakati chuo kikuu cha Oxford kikifanya jaribio la kuzuia maambukizi katika mazingira ya huduma za afya, shirika la afya duniani limetoa angalizo kuwa baadhi ya watu ambao wanajitibu wenyewe wanaweza kupata madhara makubwa.
Hazijaonekana kuwa salama na zenye uhakika wa kuzuia maambukizi ya virusi vya corona bali kuna hatari ya kupata matatizo makubwa ya moyo.
Utafiti huo umejumuisha watafiti kutoka Uingereza, Thailand, Vietnam, Laos, Cambodia na Italia.


Wednesday, May 20, 2020

MUNGU ASIKIA MAOMBI YA WATANZANIA JUU YA COVID 19

Rais Magufuli akiwa safarini kutokea Chato  alisimama mkoani Singida kuwasalimia wananchi na kuzungumza machache yakiwemo kuhusu kutakuwa na siku tatu za kumshukuru Mungu kwa Maajabu ya kutuepusha na Corona.

Saturday, July 16, 2016

LEO WATANZANIA MACHO YOTE KWA YANGA

TIMU ya Yanga leo inatupa karata yake muhimu katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuwakaribisha Medeama FC ya Ghana, mchezo utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga inayoshika mkia kwenye kundi lake la A, na inahitaji ushindi katika mchezo wa leo ili kurudisha matumaini ya kucheza nusu fainali ya michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa upande wa klabu barani Afika.
Kocha wa Yanga, Hans Pluijm amesema jeshi lake lipo tayari kwa ajili ya mchezo huo huku akijivunia kurejea kwa mshambuliaji wake Amissi Tambwe, aliyeukosa mchezo uliopita kutokana na kuwa na kadi mbili za njano alizozipata kwenye michezo iliyopita.
Uwepo wa Tambwe ni wazi utaongeza ukali wa safu ya ushambuliaji, ambayo haijafunga hata bao moja katika mechi mbili zilizopita ambazo zote wamepoteza mbele ya MO Bejaia na TP Mazembe na kuifanya timu hiyo iburuze mkia kwenye kundi lake.
Pluijm alisema amekiandaa kikosi chake kucheza kwa kushambulia zaidi ili kuhakikisha wanapata mabao mawili ya haraka kwenye kipindi cha kwanza ili kuwavunja nguvu wapinzani wao Medeama ambao wamekuja nchini wakiwa na matumaini ya kuvuna pointi tatu.
Mholanzi huyo alisema anataka kuiona timu yake ikicheza eneo la wapinzani wao kwa sehemu kubwa ya mchezo jambo ambalo litawarahisishia kupata bao muda wowote hasa kutokana na mpango wa kutumia washambuliaji watatu kwenye mchezo huo.
“Ukweli huu ni mchezo muhimu kwetu lazima tushinde ili ndoto zetu za kucheza nusu fainali ziweze kutimia ndiyo sababu tumejipanga vizuri katika muda tulioupata baada ya kucheza na TP Mazembe na ninafurahi kuona wachezaji wangu wote wapo katika hali nzuri na wanajua umuhimu wa ushindi katika mchezo huo,”alisema Pluijm.
Pluijm alisema anajua mchezo utakuwa mgumu kutokana na Medeama nao kuhitaji ushindi, lakini atahakikisha wanaitumia vizuri nafasi ya kucheza nyumbani kupata ushindi ili pia kuwafurahisha mashabiki wao ambao waliwaangusha katika mchezo uliopita kwa kufungwa na TP Mazembe.
Alisema baada ya kupoteza michezo miwili iliyopita wasingependa kupata matokeo hayo kwa sababu mipango yao ni kuhakikisha wanaanza kushinda mchezo huo na mingine iliyobaki ili kutimiza kile walichokipanga.
Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro', anatarajiwa kuanza kwenye mchezo huo akiziba nafasi ya Kelvin Yonda ambaye hatocheza mechi hiyo kutokana na kuwa na kadi mbili za njano, lakini pia kiungo Deusi Kaseke huenda asicheze kutokana na kuwa majeruhi baada ya kupata ajali ya piki piki siku za karibuni.
Kocha wa Medeama Prince Yaw Owusu, ametamba kuwa amekuja Tanzania kuchukua pointi tatu ili waweze kufufa matumaini ya kucheza hatua ya nusu fainali. Owusu, alisema anawajua vizuri wenyeji wao Yanga, na haoni kitu ambacho kinaweza kumzuia asipate ushindi kutokana na kikosi chake kuwa katika kiwango cha juu hivi sasa baada ya kufanya vizuri kwenye mechi za ligi ya Ghana.
“Najua mchezo utakuwa mgumu lakini kuijua kwangu Yanga kutasaidia kupunguza presha kwa wachezaji wangu ambao naamini hakuna anayeijua Tanzania wala Yanga yenyewe, lakini tumekuja tukihitaji pointi tatu na nina hakika wa kuzipata kwa sababu katika timu nyepesi kwenye kundi letu basi ni hii,”alisema kocha huyo.
Owusu alisema kikosi chake kitaingia uwanjani kikiwa kinawategemea zaidi viungo wa

Monday, June 20, 2016

Nape aongoza mamia kufanya Yoga

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye jana aliongoza mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam katika maadhimisho wa Siku ya Yoga Duniani kwa kushiriki kikamilifu kufanya mazoezi.
Nape aliwasili katika ufukwe wa Coco, ambapo maadhimisho hayo yalikuwa yakifanyika jana asubuhi na baada ya kuhutubia alitumia dakika kadhaa kufanya mazoezi hayo. Alikuwa na Balozi wa India nchini Sandeep Arya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambapo walipewa wasaa wao peke yao kwanza kufanya mazoezi hayo.
Baada ya hapo ilifika zamu ya watu wote waliokuwa viwanjani hapo kufanya mazoezi, ambapo pia Nape akiwa na Makonda, Balozi wa India hapa nchini pamoja na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Peter Kallaghe na wakazi wengine kuanza mazoezi hayo. Nape ambaye awali alisema kuwa alipokuwa akisoma nchini India alijifunza kwa ukaribu zaidi Yoga alionesha uwezo mkubwa wa kumudu mazoezi hayo.
Tukio hilo lililodumu kwa takribani dakika 35, ambapo waziri huyo pamoja na wenzake walifanya mazoezi hayo kwa umakini bila ya kupumzika. Walifanya mazoezi ya kunyonga miguu, kiuno, mgongo, mbavu, shingo pamoja na mazoezi mengine kama kuvuta pumzi kwa kutumia tundu moja la pua, mdomo na pamoja na mbinu nyingine za kuimarisha pumzi.
Kisha lilifuata zoezi la kunyanyua miguu juu, kufunga macho kisha kumalizia na kuomba. Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilika kwa maadhimisho hayo, Nape alisema kuwa wizara yake itahakikisha kuwa inabainisha aina ya tamaduni zenye asili ya mazoezi ndani yake na kuziendeleza.
Alisema kuwa Yoga ilianza kama utamaduni wa India, ambapo kwa sasa umekuwa ni utamaduni mkubwa duniani na umekuwa ukiadhimishwa katika kila nchi zenye ubalozi wa India. Alisema kwa kuwa Yoga inalenga kuwaweka pamoja wananchi bila ya kujali tofauti zao za kidini, kabila, uraia hata jinsia, inaendana moja kwa moja na sera ya Tanzania.
“Yoga ni moja kati ya aina bora ya mazoezi ya kufanya ambapo inasaidia kuimarisha kila kona ya mwili, na mimi nimejifunza mengi kuhusiana na Yoga wakati nikiwa India ninasoma na leo nimejikumbushia mengi sana,” alisema Nape.
Kwa upande wake Balozi wa India hapa nchini, Sandeep Arya alionesha kufurahishwa na idadi ya wananchi waliojitokeza katika ufukwe huo na kuwataka kuendelea kujitokeza kwa wingi zaidi katika kituo cha Utamaduni cha India hapa nchini kinachotoa mafunzo hayo.
Alisema kuwa Yoga ni zaidi ya mazoezi kwa kuwa yanasaidia pia kuondoa msongo wa mawazo, kukuza namna ya kufikiria mambo na pia ni njia mojawapo ya tiba kwa baadhi ya magonjwa.
“Sisi India Yoga ni utamaduni na tena ni njia mojawapo ya kujiimarisha zaidi katika maisha ya kila siku kwa kuwa kwanza ni nidhamu na pia ni mfumo wa maisha ya kila siku tunayoishi kuanzia kula na mengineyo,” alisema balozi huyo.
Aliongeza: “Kwa hapa nchini kupitia kituo cha utamaduni kilichopo chini ya Ubalozi wa India, tunatoa mafunzo kwa kila atakaye kujifunza Yoga na watu wafike kufundishwa zaidi”.
Kwa upande wake, Makonda alitoa wito wa matumizi ya lugha ya Kiswahili pia katika utoaji wa mafunzo hayo ili kila mtu aweze kuelewa kirahisi zaidi mazoezi hayo kitu ambacho kilifanyika hapo Coco ambapo mbunifu wa mavazi nchini Ally Remtulah alikuwa akitafsiri maelekezo yaliyokuwa yakitolewa na wataalamu wa Yoga kwa lugha ya Kiingereza na kuzungumza Kiswahili.
Mchezo huo umeonekana kupendwa na wengi na hata wale ambao bado hawajajiunga wameonesha nia ya kutaka kujiunga na huenda wengi wakajitokeza katika kituo hicho cha India kwa ajili ya kujifunza zaidi mchezo huo. Pia mchezo huo unaweza kumsaidia mtu kujiamini mbele ya maadui pale anaposhambuliwa na majambazi, waporaji au vibaka.

Simba wamshindwa Okwi

MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili wa klabu ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amesema hawana mpango wa kumsajili kwa mara nyingine mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda Emmanuel Okwi, kwa sababu tayari kuna wachezaji wanafanya mazungumzo nao kutoka Ivory Coast na Zimbabwe.
Hans Poppe, alisema Okwi ni rafiki yao mkubwa na anakubali uwezo wake, lakini mazingira ya kumsajili kutoka kwenye klabu yake anayoichezea hivi sasa ya Sonderjyske ya Denmark ni magumu ndiyo maana wameona kuachana naye na kutafuta wachezaji wengine ambao wapo huru na wale wa bei nafuu.
“Okwi ni mchezaji mzuri lakini kwa bajeti yetu hatutaweza kumsajili kwa sababu pesa ambazo tungemsajili yeye kutoka Denmark tuna uwezo wa kupata wachezaji wazuri tena zaidi yake kutoka mataifa ya Ivory Coast, Zimbabwe na kwingineko Afrika,” alisema Hans Poppe.
Kiongozi huyo alisema pamoja na Mganda huyo, kuichezea kwa mafanikio timu yao na kuwa na mapenzi makubwa na Simba, lakini wameona ni vyema wakaliweka swala lake pembeni huku wakipambana kutafuta wachezaji wengine ambao itakuwa ni mara ya kwanza kucheza Ligi ya Tanzania na wanahitaji kupata mafanikio ili kujenga majina yao.
Alisema wao kama viongozi wamekubaliana wasisajili wachezaji kutoka mataifa ya Uganda na Kenya kutokana na usumbufu wanaoupata mara kwa mara na hiyo ni sababu nyingine inayowafanya kuliweka pembeni jina la Okwi kwa sababu msimu ujao wamepania kurudisha heshima yao na siyo malumbano na wachezaji.
“Msimu uliopita tulikuwa na wachezaji watatu kutoka Uganda, tuliona shida yake kitu ambacho naweza kusema kimechangia kututoa kwenye mbio za ubingwa, tumejifunza na tusingependa mambo kama hayo yakajitokeza tena kwenye timu yetu ndiyo maana tumeona safari hii tubadili twende mataifa mengine yaliyopiga hatua zaidi kisoka,” alisema.
Okwi anatajwa kutaka kurudi kwenye klabu ya Simba tena hata kwa mkopo baada ya kukosa furaha kwenye klabu hiyo ya Sonderjyske, ambako ameshindwa kuwika kama ilivyokuwa Simba ambapo aliweza kupataji jina kubwa na kujizolea umaarufu wa hali ya juu na kuwa kipenzi cha wana Msimbazi.

Je unajua??

Kuwa wakwanza kuwafurahisha wakupigiao kwa kusikia muito wa jina lako pindi wakupigiapo..
Nirahisi sana unachotakiwa kufanya nikubonyeza * 148*01*4*2| alama ya reli..
Utachagua nametune kujiunga ..ukifuatia na jina lako.. kuanzia hapo marafiki zako watasikia maana ya jina lako pindi wa kupigiapo.. jaribu sasa.